Monday , 28th Nov , 2016

Muongozaji na mtayarishaji wa video nchini Hanscana amesema sababu inayopelekea video nyingi za bongo kurudiwa na kufanana ni kutokana na maamuzi na mapendekezo ya msanii mwenyewe anachopendelea.

Hanscana

 

Akipiga story ndani ya eNewz amesema "Ukiona kuna kitu kimerudiwa katika video ujue kuna makubaliano kati ya muongozaji na msanii  kwa kuwa mara nyingi msanii anapoandika wimbo wake anakuwa na wazo la aina ya video ambayo anaitaka hivyo wasanii ni kama wateja wetu na tunafanya anachokitaka mteja wetu".

Pia Hanscana amesema kwamba  yeye na Khalfani ni marafiki japo hawajawahi kufungua kampuni moja ila wakati wanatafuta maisha  waliwahi kuishi nyumba moja kwa sasa kinachowatenganisha ni kutokana na kila mmoja kuzidi kutafuta maisha yake japo bado ni marafiki.