Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanafainali wa Sprite Bball Kings waogopana

Friday , 17th Aug , 2018

Kuelekea kuanza kwa fainali ya michuano ya Kikapu nchini ya Sprite Bball Kings, timu mbili zilizotinga hatua hiyo Mchenga Bball Stars na Flying Dribblers, zimeonekana kuviziana zikisubiri kutambuana kwa mbinu kwenye game 1.

Kushoto ni nahodha wa Mchenga Mohamed Yusuf na kulia ni nahodha wa Flying Dribblers Habirmana Mayeye.

Wakiongelea 'game 1' kati ya 'best of five' ambayo itapigwa kesho Agosti 18, 2018 kwenye uwanja wa taifa wa ndani manahodha wa timu hizo, Mohamed Yusuf wa Mchenga na Habirmana Mayeye wa Flying Dribblers, wamesema wanachoweza kuahidi ni ushindani tu na mchezo ndio utaamua mshindi.

''Unajua hii ni game iliyojirudia baada ya msimu uliopita Mchenga kututoa katika hatua ya nusu fainali na hiyo ilitokana na wachezaji wetu wengi kuondoka baada ya robo fainali lakini mwaka huu tupo kamili kwahiyo tutatoa ushindani kwa bingwa mtetezi na dakika zenyewe zitaamua'', amesema Mayeye.

Kwa upande wake Mohamed amesema wao kama mabingwa watetezi wanachoweza kuwapa mashabiki ni kuendelea kuwa washindani tu kwani kabla ya ushindi huwa wanawaza namna ya kushindana na wanapoweza matokeo huwa yanakuja yenyewe.

Fainali hizo zitapigwa kwa mtindo wa 'best of five' na mshindi atajinyakulia kombe na shilingi milioni 10 huku mshindi wa pili akijipatia milioni 3 na MVP ataondoka na milioni 2. Usikose kesho kwenye uwanja wa taifa wa ndani kutakuwa na burudani nyingi na vinywaji baridi vya Sprite ambao ndio wadhamini wa michuano hii.
 

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu