Sunday , 21st Jun , 2015

Chama cha WUSHU nchini TWA kikishirikiana na ubalozi wa China wameandaa mashindano ya mchezo huo yatakayoanza kutimua vumbi Agosti 29 hadi 30 mwaka huu jijini Dar es salaam.

Katika taarifa yake, Katibu mkuu wa TWA, Gola Kapipi amesema lengo la mashindano hayo ni kuongeza hamasa ya mchezo huo hapa nchini kama ilivyokuwa kwa michezo mingine.

Kapipi amesema, michezo itakayoshirikishwa katika mashindano hayo ni Wushu, Judo, Karate, Boxing na mingine inayohusiana na ngumi ili kutoa fursa kwa michezo mingine.