Katika taarifa yake, Kocha wa Timu ya Taifa ya mchezo huo, Salum Mvita amesema, chama hicho kimeandaa mashindano hayo kwa lengo la kupata wachezaji watakaowaendeleza kwa ajili ya mashindano ya kimataifa.
Mvita amesema, wachezaji wanaotakiwa kushiriki ni kuanzia miaka tisa mpaka 24 kwa upande wa wanawake na wanaume.

