
Afisa habari wa TFF Baraka Kizuguto amesema, wanashirikiana na mamlaka mbalimbali kama vile watu wa ulinzi, usalama na hata Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU kwa ajili ya kuhakikisha mpira unachezwa kwa usalama.
Kizuguto amesema, anaamini kila mwenye kazi yake anafanya ili kuhakikisha matatizo yote yanayotokea katika mechi mbalimbali za ligi kuu yanafanyiwa kazi.