Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Goti lamponza Nadal

Tuesday , 14th Nov , 2017

Mchezaji tenisi namba moja duniani Rafael Nadal amemaliza vibaya msimu baada ya kutupwa nje ya fainali za dunia za ATP zinazoendelea jijini London Uingereza.

Mhispania huyo ameondolewa kwa kipigo cha seti 7-6 (7-5) 6-7 (4-7) 6-4 kutoka kwa David Goffin. Katika mchezo huo uliofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye uwanja wa 02 jijini London, Nadal alilazimika kucheza huku akiwa na maumivu ya goti.

Nadal aliumia goti kwenye mchezo wa robo fainali ya michuano ya Paris Masters wiki iliyopita hivyo akalazimika kujitoa ili aweze kutibiwa haraka akipigania kurejea mapema kucheza fainali za kufunga msimu huu za ATP jijini London.

Hata hivyo imekuwa ngumu kwa nyota huyo kuendelea na mashindano kutokana na kipigo hicho cha mechi yake ya ufunguzi kutoka kwa David Goffin ambaye ni raia wa Ubelgiji. Nadal amesisitiza kuwa hata kama angeshinda ilikuwa lazima ajitoe kutokana na kushindwa kuhimili maumivu ya goti.

Kuondolewa kwa Nadal kunatoa fursa kwa mkongwe Roger Federer kuisaka nafasi ya kuwa bingwa wa fainali hizo. Pamoja na kutolewa kwake lakini Nadal tayari ameshajihakikishia kumaliza msimu huu akiwa mchezaji namba moja duniani hata kama mpinzani wake mkubwa Roger Federer atatwaa ubingwa wa ATP.

HABARI ZAIDI

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani