Tuesday , 29th Nov , 2016

Msanii wa taarabu nchini Khadija Yusuph amemsihi wifi yake Leila Rashid kuachana na maswala ya muziki na kumfuata mume wake Mzee Yusuph kwa kuwa tayari mume wake kashaenda hija na ni dhambi kuacha kumsikiliza mume wake.

Khadija Yusuph

 

Akiongea ndani ya eNewz Khadija amesema ni vizuri Leila kumfuata mume wake kwa kuwa haoni sababu ya yeye kuendelea kuwa na kundi la Jahazi wakati mume wake Mzee Yusuph ameamua kumrudia Mungu na kuachana na maswala ya muziki.

Hata hivyo Khadija Yusuph amewaambia mashabiki waendelee kusubiria maamuzi ya Mzee Yusuph mwenyewe juu ya maamuzi ya mke wake kuendelea na muziki wakati yeye kaamua kumrudia Mungu na kuachana kabisa na mambo ya dunia.