Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

FAINALI DANCE 100% 2015 KUWASHA MOTO JUMAMOSI

Monday , 12th Oct , 2015

Mashindano makali ya kucheza yaliyojizolea umaarufu mkubwa Afrika Mashariki Dance 100% 2015 yanafikia tamati jumamosi hii, ambapo mshindi wa fainali hizi mwaka huu atabeba kitita cha shilingi milioni 5 za Tanzania pamoja na zawadi nyingine.

Akipiga stori na mwandishi wa habari, mtayarishaji wa kipindi cha Dance 100% kinachorushwa na EATV kila jumamosi saa kumi na mbili na nusu jioni Ndimbuni Msongole, amesema fainali za mwaka huu zitakua na mvuto kwani ni makundi matano tu yamebaki kati ya makundi hamsini.

“Mwaka huu kutakua na good show (onyesho zuri) watu wategemee vitu vizuri kwani hakuna utabiri nani atakua mshindi makundi yalikua hamsini, lakini sasa yamebaki matatu kwa hiyo washiriki watatumia uwezo wao binafsi,” alisema Ndimbuni.

Naye mtangazaji machachari wa mashindano haya ya Dance 100% yanayoandaliwa na East Africa Television na East Africa Radio, TBway 360 amezungumzia tofauti ya fainali za mwaka huu na miaka iliyopita.

“Kuna tofauti kati ya mashindano ya miaka ya nyuma na mwaka huu kwa sababu makundi mengi yamerudi baada ya kushiriki mashindano ya miaka iliyopita hivyo washiriki wengi wana uzoefu mkubwa hali inayoleta fainali yenye ushindani zaidi,” alifunguka mtangazaji huyo.

Makundi yaliyofanikiwa kuingia fainali ni fainali za Dance 100% 2015 ni The WD, Team Makorokocho, Best Boys Kaka Zao, The Winners Crew pamoja na Team ya Shamba. Fainali hizo zitatimua vumbi jumamosi hii ya tarehe 10 saa nane mchana katika viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba