Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wazazi washauriwa kutowabagua watoto wenye Ulemavu

Friday , 5th Dec , 2014

Wazazi na walezi nchini wameshauriwa kutowabagua na kuwatelekeza watoto wenye ulemavu na badala yake kuwalea kwa upendo mkubwa na kuwapa elimu kwa kuwa nao wanastahili kupewa haki sawa na wengine.

Watoto wa Shule ya Msingi Buhangija Maalum ambayo pia ni kituo cha kulelea watoto wenye Albinism.

Ushauri huo umetolewa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Buhangija Maalum ambayo pia ni kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu Bw. Peter Ajali ambapo amesema tangu serikali ilipo kiteua kituo hicho kulea watoto wenye albinism kutokana na kuzuka kwa wimbi la mauaji yao katika mikoa ya kanda ya ziwa kwa imani za kishirikina baadhi ya wazazi wamewatelekeza watoto wao kituoni hapo.

Ameyasema hayo wakati akipokea msaada wa nguo, mafuta na sabuni wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 14 kwa ajili ya watoto hao kutoka shirika lisilo la kiserikali la kikristo la kuhudumia wakimbizi (TCRAS) ambapo amesema watoto hao wamekuwa wakikosa haki zao za msingi ikiwemo malezi na upendo wa wazazi au walezi kutokana na kutelekezwa kituoni hapo kwa kipindi cha muda mrefu sasa.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Mkurugenzi wa TCRS Tanzania Mratibu wa shirika hilo Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga Bi. Rehema Samwel amesema shirika lake limeamua kutoa msaada huo baada ya kubaini kuwa hitaji kubwa la watoto hao ni nguo kwa ajili ya kujisitili, kujikinga na baridi na wenye albinism kujikinga na jua kali.

HABARI ZAIDI

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi