Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Wanawake hawaelewi rushwa ya ngono"- Mbunge Ayoub

Thursday , 24th May , 2018

Mwakilishi wa Jimbo la Paje, Jaku Hashim Ayoub ameitaka serikali kuchukua hatua za kuwadhibiti waajiri wanaojihusisha na vitendo vya kuwaomba wanawake rushwa ya ngono kwenye ajira.

Mwakilishi huyo ameyasema hayo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi wakati akiuliza swali lake la msingi kuhusu wanawake kudaiwa rushwa ya ngono na wanatakiwa wafanye nini wanapokutana na kadhia hiyo.

Akijibu swali la hilo, Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto, Shadia Mohammed amesema serikali haina takwimu za matukio hayo kwa kuwa wanawake wengi hawaelewi rushwa ya ngono ila viashira huwa vinaonekana na hushindwa kuripoti vitendo hivyo.

"Wanawake wanashindwa kuripoti matukio hayo kwa kuwa wanahofia kuachishwa kazi au kukosa kazi, kwa kawaida rushwa ya ngono hufanyika kwa siri sana tofauti na rushwa nyingine na hufanywa kwa lengo la kupandishwa cheo, mshahara au msaada wowote katika kazi", amesema Shadia.

Aidha, Shadia amesema serikali inaendelea kutoa elimu ya rushwa ili kujenga uelewa wa dhana na maana halisi ya rushwa na kuepukana na matendo hayo.

Kwa upande mwingine, Naibu Waziri huyo amewataka wanawake wanaokumbana na kadhia hiyo kuenda kuripoti Polisi pamoja na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa Zanzibar ili kudhibiti matukio hayo.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao