Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanajeshi 11 waliofariki Mbeya, tume kuundwa

Tuesday , 19th Jun , 2018

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), limesema litaunda tume maalum kwa ajili ya kuchunguza chanzo cha ajali ya gari la Igunga Trans lililoua watu 13, wakiwemo vijana 10 wa JKT, askari mmoja wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) na raia wawili iliyotokea eneo la Igodima jijini Mbeya.

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Martin Busungu

Akizungumza wakati wa zoezi la kuaga miili ya askari hao lililofanyika katika viwanja vya JKT Itende Mbeya, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini Martin Busungu, amesema mara baada ya tume kukamilisha uchunguzi wa ajali hiyo hatua kisheria zitachukuliwa kwa yeyote aliyehusika.

Akitoa salama za pole kwa ndugu na Taifa kwa ujumla kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Venance Mabeyo, Mnadhimu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni  Jenerali Yakoub Mohammed amesema taifa litawakumbuka vijana hao kwa uzalendo ikiwemo ujenzi wa ukuta wa Mererani, na kuongeza kuwa vijana waliopata ulemavu wa kudumu katika ajali hiyo Jeshi litaandaa utaratibu wa namna ya kuwasaidia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Paul Ntinika kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Amos Makalla,  amewataka watumiaji wa barabara kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepukana na ajali zinazoweza kuepukika.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea