Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yawalegezea wenyeviti wa mitaa

Tuesday , 17th Jan , 2017

Serikali imesitisha agizo lake lililokuwa linawataka wenyeviti wa Serikali za Mitaa kote nchini kurudisha mihuri katika Halmashauri za Wilaya na kuwapatia Watendaji wa Mtaa kuitumia mihuri hiyo katika shughuli mbalimbali za utendaji katika ngazi hiyo

George Simbachawene - Waziri wa TAMISEMI

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. George Simbachawene, amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa waendelee kutumia mihuri hiyo kama ilivyokuwa hapo awali mpaka pale utaratibu mwingine utakapotangazwa na kwamba uamuzi huo utawashirikisha ili kuleta ufumbuzi wa matumizi ya mihurio hiyo.

Mhe. Simbachawene amesema, hapo awali serikali ilikuja na uamuzi huo kama suluhisho la kuondokana na tabia ya wenyeviti wa serikali za mitaa wasio waadilifu ambao wanatumia mihuri hiyo vibaya kwa kuuza mali na mashamba ya kijiji, na wakati mwingine kupelekea migogoro mikubwa ya ardhi hapa nchini ikiwemo ya wakulima na wafugaji, na kutoa ardhi kwa wawekezaji kinyume cha sheria.

Aidha, Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Halmashauri ya Ubungo na Kinondoni ambaye ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwongozo Bw. James Ngoitanile amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa kote nchini kutofurahia kurudishiwa mihuri hiyo na badala yake wapime utendaji wao na kuondoa kasoro zote zinazolalamikiwa.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya