Tuesday , 22nd Apr , 2014

Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi George Simbachawene amesema kuwa serikali inapanga kutaifisha maeneo makubwa ya ardhi ambayo yako wazi na hayatumiki kwa ajili ya kukuza pato la taifa na kuwapa wakulima wayaendeleze.

Naibu waziri wa ardhi na maendeleo ya makazi nchini Tanzania mheshimiwa George Simbachawene

Waziri Simbachawene alitoa kauli hiyo wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wakulima iliyoandaliwa na mtandao wa kitaifa wa makundi ya wakulima nchini Tanzania (Mviwata) mkoani Morogoro.

Waziri Simbachawene amesema kuwa nchi hii ina eneo kubwa sana la ardhi ambalo linaweza kuwanufaisha wakulima.