Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Magufuli ashauriwa kuoa wake wawili

Saturday , 10th Dec , 2016

Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amepewa siri ya kuendelea kuwa imara kimwili hata kama atafikisha umri mkubwa kuwa ni lazima aoe wake wawili.

Rais Magufuli akihutubia katika sherehe za uhuru

Ushauri huo amepewa na Rais wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi, ambaye amefanikiwa kudumu na uimara wake licha ya kuwa na umri mkubwa kiasi cha kuendelea kuhudhuria sherehe mbalimbali za kitaifa pamoja na mialiko mbalimbali.

Rais Magufuli ndiye aliyetoboa siri hiyo jana katika hotuba yake wakati akitoa salamu za maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanzania Bara, katika sherehe zilizofanyika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Wakati akiwashukuru na kuwapongeza viongozi wakuu wa nchi waliomtangulia kwa kazi nzuri walizofanya, Rais Magufuli alimtaja Mzee Mwinyi kama mtu wa mafano katika kutunza afya yake na kwamba hata yeye alimuomba ushauri wa kitu cha kufanya ili awe kama yeye kipindi atakapozeeka.

Rais Magufuli akimsalimia Mzee Mwinyi katika sherehe za Uhuru.

 

Rais Magufuli alisema kuwa ushauri aliopewa na Mzee mwinyi ni pamoja na sharti la kuwa na wake wawili.

"Hata mimi nilipomuomba ushauri anipe siri ya kuendelea kuwa kijana hadi leo lakini akaniambia sharti la kwanza ni lazime niwe na wake wawili" Alisema Rais Magufuli.

Inawezekana Rais Magufuli aliibua suala hilo kama utani kutokana na ukweli kwamba Mzee Mwinyi mwenye umri wa miaka 91 ana wake wawili wakati Rais Magufuli ambaye ana umri wa miaka 57 ana mke mmoja kwa sasa.

Mzee Mwinyi alikuwa Rais wa Tanzania kati ya mwaka 1985 na 1995.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya