Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Odinga ajiondoa kugombea urais Kenya

Tuesday , 10th Oct , 2017

Mgombea Urais kupitia muunganiko wa vyama vya upinzani nchini Kenya, Raila Amolo Odinga, amejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho, baada ya viongozi wa Tume ya Uchaguzi Kenya IEBC, kukataa kuachia madaraka.

Akiongea na vyombo vya habari jijini Nairobi Kenya, kiongozi huyo wa upinzani ameituhumu Tume inayosimamia uchaguzi nchini humo IEBC kwa kutotaka kubadili uongozi wake, ambao wanaamini unampendelea Uhuru Kenyatta.

“Kwenye katiba ya demokrasia, hatukutakiwa kubishana kuhusu uchaguzi huru na haki, tulitakiwa kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisha tunasimamia uchaguzi huu na mfumo wake wa kielektoniki, lakini kuendelea na uchaguzi bila marekebisho kwenye IEBC ni misingi ya vikwazo kwa huu uchaguzi, uchaguzi pekee ambao Jubilee wanataka ni ule ambao lazima watashinda hata kama sio kwa sheria”, amesema Raila Odinga.

Uamuzi huo wa Raila Odinga umekuja siku moja baada ya Uhuru Kenyatta kumtaka ajitoe kwenye kinyang'anyiro kama hayuko tayari kurudia uchaguzi huo ulioamriwa na mahakama.

Pamoja na hayo viongozi hao wa NASA wameitisha maandamano ya nchi nzima hapo kesho asubuhi, ili kupinga kitendo cha Tume ya Uchaguzi kutobadili uongozi wake.

Septemba 1, 2017 Mahakama ya Juu nchini Kenya ilfuta matokeo ya uchaguzi wa Urais baada ya NASA kuishtaki IEBC kwamba walifanya udanganyifu na kukutwa na hatia, na kuamuru uchaguzi huo urudiwe ndani ya siku 60, ndipo Tume ya Uchaguzi ikaitangaza Oktoba 26 kuwa siku ya uchaguzi wa Urais.
 

 

 

 

Endelea kubaki nasi kwa taarifa zaidi.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya