Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nikihama chama wataniua

Thursday , 23rd Nov , 2017

Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam, Issaya Mwita amefunguka kuwa kamwe hafikirii kuhama Chama cha Demokrasia na Maendeleo kwa kusema kwamba hafikirii kuhama chadema kwani familia yake itateketezwa kwa mapanga na wananchi akiwepo yeye pia.

Akizungumza leo asubuhi kupitia kipindi cha EABreakfast,  ndani ya East Africa Radio, Mwita amesema kwamba amekitumikia Chadema kwa muda mrefu ikiwepo kutumia fedha zake binafsi kwenye kukijenga chama hivyo hadhani kama anaweza kuhamia chama kingine kwani hata madaraka aliyonayo anaamini yanamtosha kabisa.

Mwita amesema kwamba amesikitika sana kuona kuna baadhi ya watu waliohama vyama na kuongeza kwamba yeye ameaminiwa na wana Dar es salaam ndiyo maana akapewa dhamana kubwa ambayo ni kubwa kuliko hata nafasi ya Waziri.

"Nchi hii tumeanza kuitumikia tangu tupo majeshini. Hatukuwahi kununuliwa, lakini nawashukuru wana Dar es salaam kwa kuniamini pia nafasi niliyonayo ni kubwa. Nahama Chadema naenda wapi na nikienda huko nitafanya kazi gani? Najua kuna 'Cheap' Politics ambayo inafanyika ili kubomoa chama chetu lakini sisi tunaamini hapa tutavuka jambo hili na tutafika pazuri". Meya Mwita

Mwita amesema kwamba sifa moja ya kabila analotoka siyo watu wa kuyumbishwa hivyo siku atakapobadili msimamo ndiyo siku ambayo ataipoteza familia na yeye mwenyewe.

"Nipo ndani ya chama hiki tangu 1999. Nimekijenga kwa nguvu na pesa zangu. Hivyo naanzaje kufanya upumbavu kama huo. Nikuambie siku nikifanya uamuzi huo utasikia mama yangu amekufa, kaka zangu na hata mimi mwenyewe, Siku nikihama labda wanihamishie mbinguni lasivyo wataniua. Unataka mimi nife....aaah siwezi". amesema Mh. Mwita

Aidha, Mh. Mwita amesema kwamba aina yake ya kuliongoza jiji la Dar es salaam imekuwa tofauti sana kwani ameamua kuwa mkimya ili kuleta maendeleo kwa wananchi hivyo suala la kupiga kelele halitakuwa na tija kama hakutakuwa na maendeleo.

Msikilize hapa chini akifunguka zaidi.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea