Bwana Mhere Mwita amesema kuwa serikali ya awamu ya tano ya Dr. John Magufuli inatakiwa kuwaangalia wachimbaji wadogo wadogo wilaya Geita kwa huruma na itatue kero hiyo.
" Wachimbaji wadogo hapa wilayani wapewe sehemu ya kujichimbia dhahabu ili kuondokana na Vifo vya vijana ambao huwa wanauwawa kila siku na Askari wa Mgodi wa Geita wanapoenda kuchukua mabaki ya mawe yaliyotupwa alimaarufu kwa jina la (Magwangara)". Amesema Mwenyekiti huyo wa BAVICHA Bwana Mhere
Mhere amesema mateso kwa wananchi hao wa Geita sasa yafikie mwisho kwani kila mwananchi ana haki katika nchi yake na serikali isikie kilio cha wachimbaji hao


