Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mufindi waibana serikali kuhusu barabara

Saturday , 6th Dec , 2014

Wananchi wa vijiji vya Igowole na Mufindi Kibaoni wilayani Mufindi wameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa barabara ya Nyololo Igowole hadi Mgololo yenye urefu wa kilomita 77.6

Wananchi wa vijiji vya Igowole na Mufindi Kibaoni wilayani Mufindi wameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa barabara ya Nyololo Igowole hadi Mgololo yenye urefu wa kilomita 77.6 kwani barabara hiyo ni muhimili kwa uchumi wa wilaya ya mufindi na taifa kwa ujumla kutokana na uwepo wa viwanda vikubwa kikiwemo kiwanda cha karatasi cha mgololo.

Wananchi hao wamesema hayo kwenye mikutano ya hadhara iliyofanywa na Naibu Waziri wa Ujenzi mhandisi Gerson Lwenge wakati alipotembelea kukagua barabara na kuongea na wananchi wa vijiji vinavyopitiwa na barabara hiyo ambapo wananchi hao wamemwambia Naibu Waziri huyo kuwa wamekuwa wakiahidiwa kujengewa barabara hiyo kwa kiwango cha lami kwa muda mrefu sasa lakini utekelezaji wake umekuwa kitendawili.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi katika kijiji cha Kibaoni bwana Jacob Sanga amesema ahadi za serikali zisizoambatana na utekelezaji kujenga barabara  hiyo zinakweka chama hicho tawala katika wakati mgumu ambapo wao kama viongozi wamekosa majibu ya kuwapa wananchi wanapohoji utekelezwaji wa ahadi hiyo ya serikali.

Akijibu malalamiko hayo Naibu Waziri wa Ujenzi Gerson Lwenge amesema serikali imeshaanza hatua za ujenzi wa barabara hiyo kwa kufanya upembuzi yakinifu hivyo kuwatoa hofu wananchi hao na kwamba serikali ina thamini mchango unaotolewa viwanda vya chai, kahawa na karatasi vinavyotegemea barabara hiyo kwa ajili ya kusafirisha malighafi pamoja na bidhaa zinazotoka viwandani humo.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya