
Mjumbe wa bunge maalumu la katiba na naibu katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF (Tanzania Bara) Julius Mtatiro
Akizungumza leo na East Africa Radio, Bw. Mtatiro ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Upinzani cha (CUF) Tanzania Bara, amesema hali hiyo inachangiwa na Chama Tawala cha CCM kuhodhi mchakato mzima wa Katiba.
Mtatiro amefafanua hali hiyo imechangia matukio ya mara kwa mara ya kuvurugika kwa mchakato huo hasa baada ya wajumbe kutoka makundi mengine yenye uwakilishi katika bunge hilo kuona kuwa hayatendewi haki na wenzao wa CCM ambao amedai kuwa wamehodhi mchakato huo.