Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kaliua yaibuka kidedea mpango wa kuinua elimu

Tuesday , 17th Jan , 2017

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako amekabidhi hundi ya shilingi 704, 627,856 kwa Halmashauri ya Kaliua ambayo imekuwa ya kwanza kati ya 10 zilizofanya vizuri katika utekelezaji wa mpango wa 'lipa kulingana na matokeo'

Prof. Joyce Ndalichako 

Katika mwaka wa pili wa utekelezaji wa program hiyo ambayo iko chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (2015/2016), zaidi ya shilingi bilioni 22 zimetolewa kama motisha kwa halmashauri 179 kulingana na jinsi zilivyokidhi vigezo.

Halmashauri zilizoongoza na kiasi cha pesa kwenye mabano ni kama ifuatavyo. Kaliua (704, 627,856), Geita (657,954,115),  Bunda (538,189,807), Rorya (419,338,115), Nzega (415,222,770), Ngara (384,769,590), Itilima (364,387,825), Kongwa (363,652,691) na Chato 336,207,850)

 

Halmashauri zote 10 zilizofanya vizuri zimepewa fedha hizo baada ya kufanya vizuri zaidi kwenye maeneo mbalimbali ya malengo ikiwa ni pamoja na uandaaji mzuri wa takwimu za shule zao, urekebishaji wa ikama ya walimu kwa kuwatawanya ndani ya halmashauri kwa kuzingatia mahitaji na utawanywaji na taarifa za matumizi ya fedha za ruzuku na uendeshaji wa shule kwa usahihi na wakati.

Kwa upande wake Mkurugezi wa Halmashauri ya Kaliua, Bw. John Pima, amesema fedha walizopatiwa na serikali wanazielekeza katika utekelezaji na uboreshaji wa elimu katika halmashauri hiyo na kuongeza zaidi kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.

Kwa upande wake Waziri Ndalichako amewataka viongozi wote wanaosimamia masuala ya elimu kufanyakazi kwa weledi ili kuleta tija katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kuinua kiwango cha ubora wa elimu nchini.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya