Mshambuliaji wa Azam, John Bocco akijaribu kumtoka beki wa Mbeya City,Yusuph Abdallah
Klabu ya soka ya Azam imejihakikishia kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara baada ya kuifunga timu ya Mbeya City goli 2-0,katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya