Mkuu wa polisi nchini Tanzania IGP Ernest Mangu. Ofisi yake imetakiwa kueleza alipo rais wa jumuiya ya wanafunzi wa elimu ya juu nchini TAHLISO Musa Mdede, vinginevyo wanafunzi hao wataitisha mgomo wa nchi nzima.
Wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Tanzania wametishia kufanya mgomo usio na kikomo kushinikiza jeshi la polisi lieleze alipo mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi wa elimu ya juu TAHLISO Musa Mdede.