Wakulima wakorosho Pwani kupata ahueni
Waziri wa Kilimo,Uvuvi na Mifugo nchini Tanzania Mwigulu Nchemba atoa masaa 48 kuanzia leo kwa Kampuni ya Sparkway LTD kulipa shilingi Bilion 3.4 kwa wakulima wa Korosho wa mkoa wa Pwani na baada ya malipo hayo kufanyika wakulima wataanza kulipwa pesa zao siku ya jumatatu ijayo kwa utaratibu maalumu uliowekwa na wakulima hao pamoja na serikali.