Lipumba kushtakiwa Baraza Kuu la CUF
Kamati ya Utendaji ya Taifa ya Chama cha Wananchi (CUF), imeandaa ajenda ya kumfikisha Prof. Ibrahim Lipumba mbele ya baraza kuu la uongozi wa chama hicho ili ajieleze kwa nini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuvunja na kuvamia ofisi.