Musukuma amtaka Mpina kung’atuka
Mbunge wa Geita Joseph Musukuma (CCM), amemtaka Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhanga Mpina kujitafakari na kung’atuka kufuatia maofisa wa wizara hiyo kuingia bungeni bila ridhaa katika mgahawa wa Bunge na kupima samaki wanaodaiwa kuvuliwa haramu.