Irene Uwoya apigwa onyo
Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), imempiga onyo msanii wa filamu nchini, Irene Uwoya kwa kitendo chake cha kuchapisha picha za nusu utupu kwenye mitandao huku wakimsisitizia kuwa endapo atarudia kufanya hivyo adhabu kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.