Polisi waeleza namna mume, alivyomuua mke wake
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha linamshikilia Elibariki Geofrey mkazi wa Chekereni wilayani Arumeru, kwa tuhuma za mauaji ya mke wake Ester Elibariki, baada ya kumpiga risasi mbili kifuani na shingoni, kisha na yeye kujijeruhi nayo shingoni, na sasa anatibiwa kwenye Hospitali ya Mount Meru.