"Silinde hajaandika barua ya kujiuzulu" - Bulaya
Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Bunda Mjini Ester Bulaya, amesema kuwa Mbunge wa Momba David Silinde, hajaandika barua ya kujiuzulu isipokuwa kaamua kuachia ngazi baada ya Wabunge wenzake kutokuwa na imani naye, kwani alikiuka maagizo ya Mwenyekiti wa chama hicho.