ACT Wazalendo wamwomba Membe agombee Urais
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na wanachama wengine wamemuomba aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, kuchukua fomu ya kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao, kupitia chama hicho.

