Marais Wastaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete,na Ali Hassan Mwinyi, pamoja na Rais John Pombe Magufuli, wakiweka shada la maua kwenye kaburi la Rais Mstaafu Marehemu Benjamin Mkapa.
Safari ya Rais wa awamu ya tatu Benjamin William Mkapa, imefika tamati rasmi hii leo baada ya kupumzishwa katika nyumba yake ya milele kijijini Lupaso, Wilayani Masasi Mkoani Mtwara.