Agizo la Rais Uwanja wa Mkapa laanza kutekelezwa
Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo imeanza kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli kubadili jina la uwanja wa Taifa kumuenzi Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamini Wiliam Mkapa.

