Jumanne , 24th Sep , 2024

Mabingwa watetezi wa Ligi kuu Yanga itacheza mechi yake ya pili Ligi Kuu dhidi ya Ken Gold baada ya ile ya Kagera Sugar zote ikianzia ugenini, huku ikijivunia kutinga makundi Ligi ya Mabingwa Afrika bila kupoteza wala kuruhusu bao lolote

Wakati mashabiki wa Yanga wakitambia kikosi chao kushinda kwa idadi kubwa ya mabao dhidi ya Ken Gold, Kocha Mkuu wa timu hiyo, Miguel Gamond amesema anachotaka ni pointi tatu, lakini wapinzani wao wakijichanganya watawapiga nyingi.

"Denis Nkane kwangu namuona ana uwezo wa kuwa beki wa pembeni anayeweza kushambulia (wingback) kwasababu ana kasi na ujuzi, naamini hii nafasi itamjenga kuwa bora zaidi kwenye siku za usoni''Miguel Gamondi 
Kocha huyo ameongeza ku

wa wachezaji wote walosafiri wako fiti isipokuwa wanamkosa Farid Mussa ambaye ni majeruhi, akieleza kuwa Yanga inao nyota wengi na wenye uwezo hivyo wanasubiri muda ufike waingie uwanjani.

Kuhusu ratiba yao na hali ya uchovu, Gamond amesema hana hofu yoyote kwani wachezaji wake wanao uzoefu na uwezo binafsi na anachoweza kufanya ni kufanya maboresho