Jumamosi , 21st Oct , 2023

Malori yaliyobeba misaada yameingia Gaza kwa mara ya kwanza tangu vita vya Israel na Hamas vilipozuka.

Picha za moja kwa moja zinaonesha magari ya Umoja wa Mataifa yakiwa na bendera nyeupe yakipita katika kivuko cha Rafah kuingia Gaza kutoka Misri

Kundi la Hamas limewaachia huru mateka wake wa kwanza tangu shambulizi la kushtukiza dhidi ya Israel wiki mbili zilizopita.

Mama na binti Judith na Natalie Raanan walikuwa miongoni mwa watu 200 waliotekwa nyara; Ndugu wa kambo wa Natalie ameiambia BBC kuhusu furaha yake ya "kuzidi" wakati wa kuachiliwa kwao

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Israel inajaribu kuwaachia huru mateka zaidi, ingawa vikosi vyake pia vitapigana hadi ushindi. Israel yaendelea kushambulia Gaza usiku wa kuamkia leo

Ni wiki mbili tangu Hamas ilipoanzisha mashambulizi yake dhidi ya Israel na kuua zaidi ya watu 1,400. Maafisa wa Palestina wanasema zaidi ya watu 4,000 wameuawa Gaza tangu wakati huo.

Na viongozi wa nchi za Kiarabu na Ulaya wanakutana Misri kujadili mzozo huo, lakini matarajio ni ya chini kwa sababu wachezaji muhimu kama Iran - na Israel yenyewe - hawahudhurii