
Kaimu Mkurugenzi wa habari na uhusiano makao makuu ya JWTZ Luteni Kanali Gaudentius Ilonda
Kaimu Mkurugenzi wa habari na uhusiano makao makuu ya JWTZ Luteni Kanali Gaudentius Ilonda, akitoa tahadhari hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dodoma leo amesema baadhi wanaovaa mavazi hayo wamekuwa wakiyatumia kufanyia uhalifu na utapeli.
"JWTZ linawsihi na kuwaomba wananchi wote kusalimisha mavazi hayo ndani ya siku saba kuanzia leo na baada ya siku hizo kupita atakayekutwa nazo hatua kazi zitachukuliwa dhidi yake," amesema
Aidha Luteni Kanali ILONDA amesema licha ya wasanii wa Tanzania kuiletea mafanikio nchi lakini wanahusika na katazo hilo isipokuwa wanaweza kutumia mavazi hayo iwapo watakuwa wamepata kibali maalum.