
Akizungumza na wafanyabishara Mstahikimeya Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko, amewataka kuendelea kulipa ushuru wa huduma pamaoja na kulipia leseni zao, kutokana na fedha hizo kuwanufaisha wananchi kwa kuboresha miundombinu, badala ya kuishia mifukoni kwa watu wachache kwa maslahi yao binafsi
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha wafanyabiashara wa viwanda na kilimo (TCCIA)Mkoa wa Shinyanga Dk. Kulwa Meshack, amesema wataendelea kusimamia ili ujenzi ukamilike mapema, huku msimamizi wa ujenzi Snatus Kuchibanda amesema ujenzi utafanyika usiku na mchana
Nao baadhi ya wafanyabiashara wa soko kuu, wamesema ujenzi huo utasaidia kuboresha miundombinu iliyopo.