
Kushoto ni msanii Ibraah na mrembo Nanah, kulia ni tattoo aliyochorwa Ibraah
Akizungumzia hilo kupitia Kamera ya EATV & EA Radio Digital, Ibraah amesema kuchorwa tattoo na mrembo huyo haihusiani kwamba ndio wapo kwenye mahusiano bali kilichokuwepo kwao ni upendo na urafiki.
"Nanah sio mtu wangu ni rafiki yangu na ana mahusiano yake, kuhusu tattoo kila mtu anaamua kuchora, nilivyomuona nilimuuliza akasema amependa tu kuchora jina la Ibraah kwa sababu mimi ni mtu wake wa karibu na nina umuhimu kwake, mbona kuna watu wengi wamenichora ila wanamsema Nanah tu" amesema Ibraah
Pia ameendelea kusema urafiki wao kwa sasa una muda wa miezi 6 na kinachoendelea kati yao ni upendo tu.
Zaidi tazama hapa chini kwenye video.