Jumatano , 18th Mar , 2026

Rais wa Jamhuri ya KONGO-BRAZAVILLE Denis Sassou Nguesso ameshinda tena uchaguzi kwa asilimia 94.82 ya kura, na kuongeza awamu nyingine baada ya karibu miaka 42 ya kutawala taifa hilo.

Wanadiplomasia na wachambuzi wa kisiasa walitarajia ushindi mwepesi kwa Sassou-Nguesso, 82, ambaye alikuwa akichuana na wapinzani sita ambao hawakuwa na umaarufu sana.

Wagombea walioshindwa wana siku tano za kuwasilisha pingamizi, na Mahakama ya Katiba ina siku 15 za kuchunguza changamoto zozote kabla ya kuchapisha matokeo ya mwisho.

Vyama vikuu vya upinzani havikuteua wagombea, wakilalamikia ukosefu wa uwazi, huku wapinzani wawili maarufu Jenerali Jean-Marie Michel Mokoko na Andre Okombi Salissa, wakisalia gerezani kwa karibu muongo mmoja.