Nyota wa Golden State Warriors , Klay Thompson (Pichani chini) akiugulia maumivu alipoumia uwanjani.
Hii ni mara ya pili kwa Thompson mwenye umri wa miaka 30 kupata majeraha yatakayomuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu baada ya awali kupata maumivu ya goti kwenye mguu wake wa kushoto kwenye mchezo wa fainali ya NBA dhidi ya Toronto Raptors mwezi wa sita mwaka jana.
Kuumia kwa Klay Thompson kumewashtua wapenzi wa Golden State warriors ambao wanakumbuka msimu uliopita haukuwa mzuri sana kwao kutokana na kuumia kwake na kutocheza michezo pamoja na nyota wao mwingine Stephen Curry.