![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2020/02/02/Mwamposa1.jpg?itok=EeBOApcK×tamp=1580639375)
Waziri George Simbachawene na Mtume na Nabii Mwamposa
Tukio hilo limetokea jana, Februari 1, 2020 ambapo waumini hao walikuwa wakigombania kukanyaga 'maji ya upako' ya Mtume na Nabii Mwamposa katika Uwanja wa Majengo mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Akizungumzia tukio hilo, Waziri Simbachawene amesema serikali inafikiria kutengeneza kanuni za uanzishwaji wa huduma za kiroho kuwa lazima mchungaji awe amesomea theolojia.
Mtume Mwamposa atapelekwa mjini Moshi kwa ajili ya kufunguliwa mashtaka.