
Tangu alipoteuliwa kuwa kocha wa West Ham United Moyes, ameisaidia timu hiyo kutoka katika mstari wa timu zinazotakiwa kushuka daraja kwa kutokufungwa michezo mitatu.
"Nina uwezo wa kufanya kazi hii katika klabu yoyote duniani na nina uhakika nitalifanya hili nikiwa na West Ham," alisema kocha huyo.
Kocha huyo raia wa Scotland mwenye umri wa miaka 54, anajaribu kurudisha heshima yake baada ya kufanya vibaya alipoviongoza vilabu vya Manchester United, Real Sociedad na Sunderland.
West Ham kwa sasa iko nafasi ya kumi na tano katika msimamo wa ligi kuu ya nchini England.