
Katika ziara hiyo Mhe. Rais Magufuli atafungua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.
Leo asubuhi Mhe. Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi la kiwanda cha kutengeneza vigae (Tiles) cha Tanzania Goodwill Ceramic Tiles Ltd. kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani na baadaye ataelekea Mkoani Lindi.
Kesho tarehe 03 Machi, 2017 Mhe. Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani Lindi na keshokutwa tarehe 04 Machi, 2017 atafanya ziara yake Mkoani Mtwara.