Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TFF yasaini mkataba wa miaka mitano na UNFPA

Jumatano , 16th Nov , 2022

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeingia mkataba wa ushirikiano kwenye mambo ya kijamii na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshugulikia idadi ya watu pamoja na afya ya uzazi (UNFPA).

Lengo kuu la makubaliano hayo ni kurudisha kwa jamii na kuifanya Tanzania iwe sehemu salama kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ikilenga kutokomeza vifo vinavyozuilika wakati wa uzazi, kutokomeza maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi, kuzuia ndoa za utotoni na kuhakikisha malengo ya kila kijana yanafanikiwa.

Akizungumza katika hafla hiyo ya utiaji saini Rais wa TFF Wallace Karia alisema ni faraja kubwa kwa TFF kuendelea kupata wadau mbalimbali katika kufanikisha kampeni zenye lengo la kuikomboa jamii kutoka katika vitendo vya unyanyasaji na vifo kwa wanawake wakati wa kujifungua.

“Hii si mara ya Kwanza kwa TFF kufanya kampeni zinazoigusa jamii moja kwa kwa moja, tumekuwa na kampeni nyingi ikiwemo ‘Nyumba ni choo’ ‘Sensa ya watu na makazi 2022’ na nyinginezo. Hivyo kwa kushirikiana na UNFPA tutahakikisha tunaifikia jamii kwa kuwaelimisha madhara yatokanayo na ndoa za utotoni, lakini pia uzazi wa mpango na faida zake tukizielekeza kampeni hizo katika mashindano yetu mbalimbali kuanzia ligi ya vijana, ngao ya jamii na hata mitandao ya kijamii ambayo tunaamini inawafikia watu wengi” amesema  Karia.

Naye mkurugenzi mkazi wa UNFPA Mr. Mark Bryan Schreiber aliushukuru uongozi wa TFF kwa makubaliano waliyofikia na kusema kwamba TFF ni sehemu Sahihi ambayo itaifikia jamii kwa urahisi kupitia mchezo wa mpira wa miguu ambao unapendwa na watu wengi duniani. Kwani anaamini kupitia kampeni mbalimbali zitakazofanywa na wachezaji pamoja na wadau mbalimbali wa TFF zitaleta mabadiliko chanya kwa jamii

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto