Jumapili , 28th Jul , 2024

Kikosi cha Yanga kimetwaa kwa kishindo ubingwa wa mashindano ya Kombe la Toyota, jijini Bloemfontein, Afrika Kusini baada ya jioni ya leo Jumapili kuibuka na ushindi mnono wa mabao 4-0 dhidi ya wenyeji Kaizer Chiefs.

Mabao yaliyoipa Yanga ubingwa, katika mchezo huo yamefungwa na Prince Dube dakika ya 24, Clement Mzize dakika ya 62 huku Stephane Aziz Ki akipachika mawili dakika ya 45 na 62.

Kichapo hicho kinakuwa cha kwanza kwa aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi aliyekabidhiwa kikosi hicho hivi karibuni, baada ya kuachana na FAR Rabat ya Morocco aliyoachana nayo kufuatia kukosa ubingwa wa Ligi ya Morocco 'Botola Pro'.