Wachezaji wa Yanga wakifanya mazoezi yao leo katika uwanja wa Uhuru Jijini Dsm.
Katika mazoezi hayo Kocha Mkuu mwenye uraia wa Zambia, George Lwandamina ameonekana kukinoa kikosi hicho kipya kikiwa na wachezaji wapya kama Ibrahim Ajibu na Abdallah Haji Shaibu 'Ninja'.

Katika hatua nyingine, Yanga imesajili mlinda mlango mpya Youthe Rostand raia wa Cameroon miaka miwili akitokea klabu ya African Lyon hivi karibuni ili aweze kusaidiana na Beno Kakolanya baada ya zile tetesi zikidai Ally Mustafa kuondoka kwenye kikosi hicho cha Jangwani na amekuwa akihusishwa kujiunga na Singida United.



