Alhamisi , 19th Sep , 2024

Kikosi cha Yanga SC kimeondoka Leo Alhamsi ya Septemba 19,2024 kuelekea Visiwani Zanzibar kwaajili ya mchezo wa marudiano wa mkondo wa pili wa mashindano ya. Ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya CBE ya Ethiopia utakaochezwa jumamosi hii katika uwanja wa New Amaan Complex

Mabingwa hao watetezi wa Tanzania Yanga SC katika mchezo wa mkondo wa Kwanza  waliondoka na ushindi wa bao 1-0 katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa  Abebe Bikila Addis Ababa huku mshindi yoyote atakuwa amekata tiketi ya kutinga makundi ya michuano hiyo.