Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Usajili wa Ngoma, Azam FC yatoa neno kwa Yanga

Jumapili , 27th Mei , 2018

Klabu ya soka ya Azam FC ambayo jana imekamilisha usajili wa aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga, Donald Ngoma, imerejesha shukrani kwa viongozi wa Yanga kwa kutoa ushirikiano na kufanikisha usajili huo.

Msemaji wa Azam FC Jaffar Idd Maganga, ameeleza kuwa viongozi wa Yanga wameonesha ukomavu mkubwa kwenye masuala ya michezo baada ya kubariki kwa asiliia zote uhamisho wa Ngoma kutoka kwenye klabu yao na kwenda Azam FC.

''Niwapongeze tu viongozi wa Yanga kwa kuweka wazi suala la usajili wa Ngoma kuwa walikuwa wamemalizana naye na taratibu zote zimefuatwa, ni jambo la kiungwana sana ambapo hata sisi tuliwahi kufanya hivyo kwenye usajili wa Gadiel Michael'', amesema.

Mbali na hilo Azam FC pia imeweka wazi kuwa usajili wa Ngoma ni mwanzo tu ila mashabiki wasubiri masika ya usajili yanayokuja ambapo timu yao itakuwa tishio msimu ujao wa 2018/19.

Azam FC kesho usiku itakuwa mwenyeji wa Yanga kwenye mchezo wa ligi kuu soka Tanzania Bara, ambao utakuwa ni wa kufunga pazia la ligi msimu huu huku pia timu hizo zikiwania nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala