
Juma Mahadhi ndiye aliyefunga bao la Coastal Union huku Mohammed Mtindi naye akiwafungia Wana Kimanumanu bao lao.
Wakati huo huo, JKT Ruvu wamewapa somo la “kijeshi” maafande wa Tanzania Prisons kwa kuwachapa mabao 4-1 katika muendelezo wa michuano ya Ligi kuu.
Mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam, Samwel Kamuntu alifunga bao moja, Mussa Juma akatupia moja na Michael Aidan akifunga mawili huku lile la Prisons likifungwa na Mohammed Mkopi.