
Akizungumza jijini Dar es salaam, Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli nchini CHANETA, Anna Kibira amesema, kikosi kimejiandaa vizuri kwa ajili ya mashindano hayo na ana amini kwa maandalizi waliyoyafanya wachezaji.
Kibira amesema, anaiomba Serikali kuisaidia timu hiyo kwa ajili ya malazi kwani kiasi walichokipata mpaka sasa hakijakidhi majitaji ya timu hiyo ambayo yanaweza kuwasaidia kwa ajili ya kuweza kufanya vizuri zaidi katika mashindano hayo.