
Haji Manara
Mkuu wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Haji Manara amesema klabu hiyo imeamua kukubali ombi la baraza hilo, ili kuweka mambo sawa kuelekea mkutano huo na kutoa ufafanuzi kwa jambo lolote ambalo litakuwa halijaeleweka kuelekea katika mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji wa timu hiyo.
Manara amesema kuwa kikao hichokimepangwa kufanyika wakati wowote kati ya leo au kesho, na kwamba uongozi una imani kubwa kwamba wataelewana, huku akisisitiza kuwa mkutano mkuu wa klabu hiyo uko palepale, na tayari maandalizi yamekamilika.
Katibu wa Baraza la Bodi la Wadhamini wa Simba, Hamisi Kilomoni (katikati) akizungumza na wanahabari wiki iliyopita
Wiki iliyopita baraza hilo la wadhamini la Simba lilizungumza na wanahabari na kueleza malalamiko yake kuhusu mchakato wa mabadiliko ndani ya klabu hiyo, ambapo mwenyekiti wake Mzee Hamis Kilomoni alidai kuwa Baraza hilo haljashirikishwa katika hatua yoyote ikiwa ni pamoja na mkutano huo wa dharura, na kutishia kuuzuia endapo viongozi wa Simba hawatazungumza na wajumbe wa baraza hilo.