Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mohamed Mchengerwa
Waziri Mchengerwa amewataka wachezaji hao kuweka bidii na kufata maelekezo ya walimu huku akiwa na imani kubwa na kikosi hicho kufanya vizuri kwenye mashindano hayo pamoja na kurejea na kombe hapa nchini
''Tunawaamini sana hakika mtakwenda kupambana na kuhakikisha mnafanya vyema katika kuitangaza nchi yetu katika mashindano hayo ni makubwa '' amesema Waziri Mchengerwa
Katika hatua nyingine Waziri Mchengerwa amemtambulisha rasmi Kaimu Mkurugenzi wa Michezo Ally Mayai Tembele huku akitoa wito kwa wadau wa michezo kumpa ushirikiano ili kuendeleza sekta ya michezo hapa nchini
Fainali za kombe la dunia kwa wasichana chini ya umri wa miaka 17 zinataraji kuanza Oktoba 11 mpaka oktoba 30,2022 huku Serengeti Girls ikipangwa kundi D pamoja na timu za Japan,Canada na Ufaransa