
Kamishna wa polisi wa kanda maalum ya Dar es salaam, Kamanda Suleiman Kova amesema kuwa awali wakati mechi ikiendelea, shabiki huyo Deodatus Isaya mwenye miaka 48 mkazi wa kipunguni A jijini Dar es salaam alianguka ghafla na kuonekana kama amezirai, lakini baadae aligundulika amekwishafariki
Kamanda Kova ameongeza kusema kuwa, baada ya uchunguzi huo kwa kushirikiana na madaktari watatoa majibu ya kile kilichomsibu shabiki huyo na kusababisha kifo chake.
